Monday, September 1, 2014

Brendan Rodgers amfagilia Super Mario Balotelli

Rodgers: Super Mario Balotelli Anastahili Pongezi (Video)
Meneja wa klabu ya Liverpool Brendan Rodgers amempa tano mshambuliaji mpya wa klabu hiyo Super Mario Balotelli kufuatia uwezo safi aliouonyesha wakati wa mchezo wa ugenini dhidi ya Tottenham Hotspurs.
Rodgers ambaye alikishuhudia kikosi chake kikicheza mchezo wa 100 tangu alipoanza kazi huko Anfield miaka miwili iliyopita amesema kwa hakika Balotelli alionyesha soka safi na anaamini ilikuwa tofauti na ilivyokuwa inatarajiwa na mashabiki wengi.
Amesema mara nyingi huwa ni vigumu kwa mchezaji yoyote kucheza vizuri katika mchezo wa kwanza hasa ikizingatiwa Balotelli alimsajili mwanzoni mwa juma lililopita akitokea nyumbani kwao Italia alipokuwa akiitumikia klabu ya AC Milan.
cheki alichokisema hapo chini;



No comments:

Post a Comment