Wednesday, August 6, 2014

Linex atangaza nia ya kugombea ubunge 2020 kupitia chama kipya



Linex Sunday Mjeda ameingia kwenye orodha ya baadhi ya wanamuziki wa Tanzania ambao tayari wameamua kuweka wazi  nia na mipango waliyonayo ya kujihusisha moja kwa moja na  mambo ya siasa .
Akizungumza na Soudy Brown katika U Heard ya Clouds FM ya Agosti 6, Linex amesema amejiunga na chama kipya kiitwacho ACT , na ana mpango wa kugombea ubunge ifikapo mwaka 2020.
Linex  amesema  ameamua  kujiunga na chama hicho kipya kumsupport mbunge maarufu Zitto Kabwe
Ndio mwenyekiti wetu na tuta deal nae, kwasababu ni kijana kama sisi, ana support mipango yetu so hakuna sababu yoyote ya kushindwa kumsupport kijana mwenzako. Kwahiyo mimi nitamsupport Zitto kwasababu ana support mipango yangu pia kwahiyo I’am in, ACT baby”. Alisema Linex

No comments:

Post a Comment