
‘Mimi na Yanga tulikua na makubaliano ya mkataba na hakuna ukweli kwamba Mshahara niliokua nalipwa Yanga ni mdogo, mshahara usingekua unatosha nisingekubali kusaini mkataba‘
‘Ni kweli kuna mambo mengi hayapo sawa kati yangu na club yangu yaYanga ila ni
mambo ya ndani ambayo nisingependa kuyazungumzia, ni mambo madogo ambayo
nadhani yanaweza kuisha‘
‘Hakuna
ukweli kwamba mimi nakwenda Ulaya, sijui hata imetoka wapi na nani kaanzisha
hii ya Ulaya, mimi bado ni mchezaji halali wa Yanga na huwa naongea nao karibu
kila siku, hata jana nimetoka kuongea na katibu mkuu na mambo yote yanaelekea
vizuri hamna shida yoyote mpaka sasa hivi‘ - Hii ni kauli ya mshambuliaji
wa Yanga, Emmanuel Anord Okwi.
No comments:
Post a Comment