Wednesday, August 13, 2014

Baba aua mwanaye kwa kipigo



Jeshi la Polisi Wilaya ya Sumbawanga, mkoani Rukwa, linamtafuta mkazi wa malangali, Bw.Simon Paskali kwa kosa la kuwapiga watoto wa, kumuua mmoja na kukimbia pasikojulikana.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana babaada ya mtuhumiwa kurudi nyumbani akitokea kwenye sherehe ya komunio akiwa amelewa na kuanza kuwapiga watoto wake kwa fimbo hadi wakazirai.
Akizungumzia Tukio hilo , Kaimu kamanda wa wa polisi  mkoani Humo, Frednand Rwegasila, alisema mtuhumiwa alikuwa akiishi na watoto muda mrefu baada ya kuachana na mkewe.
Aliwataja watoto hao kuwa ni Daniel Paskali(11) ambaye ndiye aliyefariki na Jackson Paskali(9) ambao baada ya kuzirai kwa kipigo na mtuhumiwa kukimbia, majirani walikwenda kutoa msaadawa kuwapeleka hosptali.
“Wakiwa njiani, Daniel alifarikidunia wakati Jackson amelazwa katika Hospitali ya mkoa akiendea kkupatiwa matibabu na ameumizwa sehemu mbalimbali za mwili wake.”Alisema
Kamanda Rwegasila alisema jeshi hilo linaendelea kumsaka mtuhumiwa ali aweze kufikishwa mahakamani

No comments:

Post a Comment