Katika
mapambani kwenye maisha watu wengi huwa wanajiuliza maswali mengi, mojawapo ni
kwa nini sifanikiwi? Kwa nini mimi tuu? Na wewe unaweza kuwa ni mmoja wao.Leo
nataka nikufahamishe jinsi ya kufanikiwa maishani na kubadili kabisa maisha
yako.Zifuatazo ni njia zitakazo kuwezesha wewekufanikiwa maishani.
1.Acha
kulaumu wengine na kujitetea.
Haijalishi
kama tatizo linalokukabili limesababishwa na nani, ama wewe au mtu mwingine cha
msingi ni kupata ufumbuzi wa tatizo.Wengi wetu tatizo likitoke huwa tunakimbilia
kuwalaumu wengine na kujitetea kwa njia hii hautaweza kufanikiwa maishani.
Elewa kwamba umebeba dhamana ya maisha yako mwenyewe na hakuna mtu yeyote wa
kubadilisha maisha yako ila wewe mwenyewe.
Pale
tatizo linapotokea kitu cha kwanza na cha msingi ni kutafuta chanzo cha chake
na kuanza kulitatatua mara moja.
2.Acha
kusitasita/Acha tabia ya kuahirisha mambo.
Unapokuwa
unataka kufanya kitu, usiwe na tabia ya kuahirisha bila sababu ya msingi.Kwa
kufanya hivi hutafanikiwa kwa sababu mambo yako uta kuwa unayafanya kwa maneno
kuliko vitendo.
Ukitaka
kufanikiwa maishani usiwe na tabia ya kuahirisha kila kitu kwamba ntafanya
kesho, kumbuka kesho huwa haifiki daima! Jitahidi kufanya mambo yako muda
huohuo.Tambua kwamba matendo ndo kila kitu katika maisha.
3.Tambua na Kuza
kipaji chako.
Utafiti
unaonyesha kuwa watu wengi hawajafanikiwa katika maisha kwa sababu wanafanya
kazi zisizoendana na ujuzi wao.Kitu kikubwa katika maisha ni kutambua ujuzi
wako.kila mtu duniani ameumbwa na kipaji fulani ama anao uwezo wa kufanya shughuli
fulani vizuri zaidi yaani kwa urahisi kuliko nyingine. Ukitambua shughuli
unayoweza kiuifanya kwa urahisi kuliko nyingine na hata saa nyingine unaweza
kushangaa uliijifunza vipi, tambua hicho ndicho kipaji chako na fanya kila
linalowezekana kukikuza na kukiendeleza.
4.Kuwa na malengo.
Kuweka
malengo na mikakati ya kutimiza hayo malengo ni jambo kubwa na la msingi
katika maisha.Watu wengi huwa wanaweka malengo bila kuweka mikakati ya kuyafikia
malengo yao.Kwa kufanya hivi ni sawa na kijidanganya.
Kinachotakiwa
ili ufanikiwa lazima uweke malengo na mikakati ya kufikia malengo hayo. kuweka
malengo kunahitaji kujipa muda pia wa kuyatimiza malengo hayo.Ili kufikia
malengo yako kirahisi unatkiwa kuwaza kama vile una muda mfupi wa kuwa hapa
duniani
Kwa maoni au ushauri tuma; bongoleotz@gmail.com.
Kwa maoni au ushauri tuma; bongoleotz@gmail.com.
No comments:
Post a Comment