Akizungumza na Bongo5 leo, Afande amedai
kuwa bila uzembe wa madaktari huenda malaria isingechukuauhai wa Mama Tunda.
“Mama Tunda ametuachia pengo kubwa sana
kwenye familia,” amesema Afande. “Amefariki jana saa tano usiku katika
hospitali kubwa hapa Morogoro kutokana na uzembe wa madaktari. Walimpa matibabu
akarudi nyumbani, sitaki kulizungumzia kiundani kwa sasa hivi kwa sababu tupo
kwenye wakati mgumu. Huku mazishi yatafanyika kuanzia kama saa tisa hivi lakini
bado hatutajua itakuwa wapi bado tupokwenye mipango. Malaria ilimchukua sana,
kwa familia na watoto kwetu ni msiba mkubwa sana, yaani ni huzuni sana,”
ameongeza Afande.
source:Bongo5

No comments:
Post a Comment