Tukio
la utupaji wa viungo vya binadamu jalalani, linalodaiwa kufanywa Chuo cha Kimataifa cha Matibabu na Teknolojia
(IMTU) cha Dar es Salaam, linadaiwa kuandika historia mbaya nchini.
Wakati
serikali ikiendelea kuchunguza tukio
hilo, ikiwemo kuunda tume nyingine chini ya Wizara ya Afya na Ustawi,
kujiridhisha kabla ya hatua
kuchukuliwa,Baraza
la Madaktari limetwishwa mzigo wa kuhakikisha
linachukua hatua kali kwa watakaobainika kuhusika na kitendo hicho Serikali
imetumia nafasi hiyo kuonya vyuo
vingine, kwa kusema jambo hili ni la
kusikitisha, la aina yake katika historia ya mafunzo ya udaktari
tangu
yaanze nchini takribani miaka 40 sasa.
"Pia
tunatoa onyo kwa vyuo vingine, mafunzo
haya tumeanza miaka 40 iliyopita lakini haijawahi kutokea kitu cha aina hii, ni
mara ya kwanza ni jambo la kusikitisha sana,"
alisema Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi, Dk Steven Kebwe
Naibu
Waziri aliwaambia waandishi wa habari kuwa kitendo hicho cha kutupa
viungo
vya binadamu hadharani, si jambo la kawaida, ni la uvunjifu wa haki za
kibinadamu.
Katika
kile kinachodhihirisha chuo hicho kung’ang’aniwa, kabla ya kuamua hatua
za kuchukua dhidi yake, Wizara hiyo yenye
dhamana ya afya, pia imeunda kamati ya
watu 15 kwa ajili ya kuchunguza tukio hilo.Kamati hiyo ya wizara iliyopewa siku saba kukamilisha
kazi, imeundwa kukiwa na tume nyingine iliyoundwa na Polisi Kanda ya Dar es
Salaam, kuchunguza
sakata
hilo la kutupwa viungo katika maeneo ya Bonde la Mbweni Mpiji, Bunju jijini Dar
es Salaam.
Dk
Kebwe aliwaambia waandishi wa habari kwamba kamati hiyo ya wizara itafanya kazi
yake kwa siku saba kuanzia juzi. Inajumuisha wataalamu mbalimbali kutoka Ofisi
ya Mkemia Mkuu, Polisi na Wizara ya Afya na Ustawi.
Aidha,
alisema zipo sheria zinazoelekeza namna ya kuteketeza miili hiyo baada ya
kumalizika kwa kazi yake.
“Lakini
inasikitisha kuona miili hiyo ilitelekezwa na watu wanaojua maadili ya kazi ya
udaktari,” alisema.
Alisema
kwa kuwa madaktari huwa wanakula viapo
baada ya kumaliza mafunzo yao,
Baraza
la Madaktari nchini linatakiwa kuhakikisha linachukua hatua kali kwa
watakaobainika kuhusika na kitendo hicho.
Timu
iliyoundwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, imejielekeza
kuja na majibu kadhaa,ikiwa ni pamoja na kufahamu idadi kamili ya watu wenye
viungo hivyo.Ikiwa na watu saba akiwemo.Mkemia Mkuu wa Serikali, itakuja na majibu
yanayofafanua viungo hivyo ni vya muda gani na zilitumika kemikali gani kuvikausha.
No comments:
Post a Comment