MKE
na mume, wakazi wa Sombetini jijini Arusha wanatuhumiwa kukutwa
na
mabomu saba ya kutupa kwa mkono aina ya grumeti , unga wa baruti,
risasi
vikihusishwa na matukio ya ulipuaji mabomu jijini hapa.
Wakati
wanandoa hao, Yusuph Ally (30) na mkewe, Sumaiya Juma (19),
wakishikiliwa
na Polisi, pia watu sita akiwemo mwalimu wa shule ya
msingi,
walinzi watatu na mfanyabiashara, wanashikiliwa kwa tuhuma za
kuhusika
katika ulipuaji wa mghahawa wa Vama Traditional Indian Cuisine,
jijini hapa.
Kuhusu
wanandoa hao wanaotuhumiwa kukutwa na silaha hizo, Mkurugenzi
wa
Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Issaya Mngulu alisema
walikamatwa
juzi usiku nyumbani kwao.
Mngulu alisema polisi katika mwendelezo wa
kusaka watuhumiwa wa
ulipuaji
mabomu, inashikilia watu hao kupata taarifa zaidi ni wapi
mabomu
hayo yametoka.
Mngulu
ambaye alitoa taarifa hiyo jana kwa waandishi wa habari jijini
hapa, alisema moja kati ya mabomu
yaliyokamatwa, kwa mujibu wa
wataalamu,
limetoka Ujerumani na yaliyobaki yametengenezwa Urusi.
“Bado
tunawashikilia watu hawa ambao ni mke na mume ili kujua mabomu
haya
walikuwa nayo ni ya nini. Pia bado tunafuatilia watu wengine
wanaohusika
na ulipuaji wa mabomu na nasema hivi hatutaishia hapa
tutaendelea
na upelelezi wetu hadi kieleweke,’’ alisema Mngulu.
Kwa
mujibu wa Mngulu, mtuhumiwa Yusuph (mume), ni miongoni mwa
waliokuwa
wakitafutwa kwa tuhuma za ulipuaji wa mabomu jijini Arusha.
Alisema mtandao wa wanaohusika na mabomu ni
mkubwa, huku watu zaidi
ya
25 wakiendelea kutafutwa na wengine 25 wanashikiliwa na Polisi. Muda
wowote
watafikishwa mahakamani.
Ulipuaji
mgahawa Wakati huo huo, Mngulu ametaja watu sita
wanaotuhumiwa
kuhusika katika ulipuaji wa mgahawa wa Vama Traditional
Indian
Cuisine. Katika mlipuko huo wa hivi karibuni, watu wanane
wakiwemo
wanne wa familia moja, walijeruhiwa.
Watuhumiwa
hao ni aliyekuwa mlinzi wa mgahawa huo, Shaban Mmasa (26)
na
Athuman Mmasa (38) ambaye ni mlinzi wa mgahawa wa Chinese uliopo
Gymkhana,
jirani na Vama Traditional Indian Cuisine.
Wengine ni Mwalimu wa Shule ya Msingi
Olturnet, Jaffar Lema (38)
ambaye
alikuwa Imam wa Msikiti wa Quba mjini Arusha. Mwalimu huyo
anatuhumiwa
miongoni mwa viongozi walioratibu matukio ya mabomu maeneo
mbalimbali.
Watuhumiwa
wengine ni Abdul Salim (31) ambaye ni wakala wa mabasi
jijini
Arusha, mfanyabiashara Said Temba (42) mlinzi wa mgahawa wa
Chinese,
Mohamed Nuru (30).
Katika
hatua nyingine, Polisi imesema inamtafuta Yahaya Hella (35),
mkazi
wa Mianzini, akituhumiwa kuhusika na ulipuaji wa mabomu nchini.
Anadaiwa
kuwa mtaalamu wa kung fu.
Hata
hivyo, DCI alikanusha kuwa baadhi ya watuhumiwa wanaokamatwa
wanahusishwa
na mgogoro wa Msikiti wa Masjid Quba. Alisisitiza kukamatwa
kwa watuhumiwa hao hakuhusiani na masuala ya
imani
Source:Habari Leo
No comments:
Post a Comment